Header Ads

Man United yaongoza timu kwa thamani kubwa kwenye soka



http://www.squawka.com/news/wp-content/uploads/2017/01/Manchester-United-e1483867552181.jpg



TIMU inayocheza soka ya Marekani Dallas Cowboys, imetetea umaarufu wake kama timu ya michezo iliyo na thamani ya juu kulingana na jarida la Forbes.
Manchester United ambayo ni miongoni mwa timu zilizotajwa kuwa na thamani ya juu mwaka 2011 na 2012, imepanda juu klabu ya Barcelona na Reala Madrid kama timu yenye thamani kubwa katika soka ikiwa na thamani ya dola bilioni 3.69.
Hatua hiyo inaiweka United katika nafasi ya 3 kwa jumla.
Thamani ya Dallas Cowboys iliongezeka kwa asilimia 5 hadi dola bilioni 4.2 huku klabu ya mpira wa baseball New York Yankees ikiwa ya pili na thamani ya dola milioni 3.7.
Hata hivyo, timu ya Los Angeles Rams ndio iliyopata faida kubwa na hivyo kupanda kutoka timu hamsini bora hadi nafasi ya 12 baada ya thamani yake kupanda maradufu hadi dola bilioni 2.9 kufuatia hatua yao ya kuondoka St Louis mwaka uliopita.
“Kuhama huko pamoja na uwanja mpya kumesababisha kuongezeka kwa thamani ya timu za NFL,” alisema Kurt Badenhausen, mhariri mkuu wa jarida la Forbes.
Timu za ligi ya NFL zilikuwa katika nafasi ya 29 miongoni mwa timu hamsini bora isipokuwa Cincinnati Bengals, Buffalo Bills na Detroit Lions ambazo hazikushirikishwa.
Hakuna timu hata moja ya kuteleza barafuni, ama hata ile ya magari ya langalanga ya Formular one iliorodheshwa.
Orodha ya timu 10 zenye thamani ya juu duniani:
  • 1. Dallas Cowboys $4.2bn (£3.26bn) American football
  • 2. New York Yankees $3.7bn (£2.87bn) baseball
  • 3. Manchester United $3.69bn (£2.86bn) football
  • 4. Barcelona $3.64bn (£2.82bn) football
  • 5. Real Madrid $3.58bn (£2.78bn) football
  • 6. New England Patriots $3.4bn (£2.64bn) American football
  • 7. New York Knicks $3.3bn (£2.56bn) basketball
  • 8. New York Giants $3.1bn (£2.4bn) American football
·          9. San Francisco 49ers $3bn (£2.33bn) American football
·         10. Los Angeles Lakers $3bn (£2.33bn) basketball

No comments

Powered by Blogger.