Header Ads

Jioni Njema; City wajitosa kwa Mbappe, wamnyakua Walker # Makelele ndiye aliyefanikisha dili la Bakayoko # Perisic haendi kokote



http://i1.mirror.co.uk/incoming/article10117137.ece/ALTERNATES/s615/Frances-Kylian-Mbappe-in-action.jpg

LONDON- MCHAMBUZI mkongwe wa soka la Hispania, Graham Hunter, amesema kuwa klabu ya Manchester City inafanya kila liwezekanalo ili kuinasa saini ya staa wa Monaco, Kylian Mbappe, kwa dau ambalo bado halijawekwa wazi. Sky Sports.
http://a.espncdn.com/combiner/i/?img=/photo/2017/0406/r197091_1296x729_16-9.jpg&w=738&site=espnfc
Mkurugenzi wa michezo wa Inter Milan, Piero Ausilio, amewakata ‘maini’ Manchester United kwa kusema kwamba windo lao, Ivan Perisic, kamwe haliwezi likajiunga nao. Sky Sports.
http://cdn3-i.hitc-s.com/380/tottenhams_kyle_walker_in_action_267081.jpg
Manchester City imekubali kutoa dau la pauni milioni 50 (sh bilioni 145), kama ada ya uhamisho wa Kyle Walker wa Tottenham. Hata hivyo, imeelezwa kuwa dau hilo linahusisha ziada (kipengele cha Man City kulipa zaidi). Sky Sports.
http://www.informationng.com/wp-content/uploads/2017/01/claude.jpg
Imebainika kuwa mchezaji wa zamani wa Chelsea, Claude Makelele, amesaidia kwa kiasi kikubwa kukamilika kwa dili la usajili la kiungo wa Monaco, Tiemoue Bakayoko. Sky Sports.
https://www.thesun.co.uk/wp-content/uploads/2017/05/nintchdbpict0003205079213.jpg?strip=all&w=960&quality=100
AC Milan imeliweka jina la Leonardo Bonucci kwenye nafasi ya kwanza, ya orodha ya wachezaji watakaosajiliwa muda wowote kuanzia sasa. Hilo linakuja, baada ya beki huyo kuzozana na kocha wake Juventus, Massimiliano Allegri. Sky Sports.
http://thesefootballtimes.co/wp-content/uploads/2015/11/o-gylfi-sigurdsson-facebook.jpg
Kiungo wa Swansea, Gylfi Sigurdsson ameikosa ziara ya timu yake nchini Marekani kutokana na kuachwa kukamilisha dili la kwenda Everton. Lakini inadaiwa kuwa dau la pauni milioni 40 (sh bilioni 116) ambalo lilitolewa na Everton limekataliwa. Sky Sports.

No comments

Powered by Blogger.