Jioni njema; Perisic apanga maisha Man Utd # Walcott kupigania namba Arsenal # Pochettino amtaka kinda wa Argentina

MILAN-
KIUNGO mshambuliaji wa Inter Milan, Ivan Perisic (28) ameonekana kupanga namna maisha
yake ya soka yatakavyokuwa ndani ya Manchester United na anatarajiwa
kukamilisha dili na kujiunga na timu hiyo kabla ya dirisha la usajili
kufungwa. Manchester Evening News.

Mshambuliaji
wa washika bunduki wa London, Arsenal na Uingereza, Theo Walcott, anatarajiwa
kupambana kwa ajili ya kupata nafasi ya kuwepo kwenye kikosi cha kwanza cha
timu hiyo licha ya kuhusishwa na usajili wenye thamani ya pauni milioni 20 (sh
bilioni 58) kwenda West Ham United. Daily
Star.
Kocha
wa Tottenham Hotspurs, Mauricio Pochettino, anadaiwa kuvutiwa na mlinzi wa timu
ya Estudiantes ya Argentina, Juan Foyth (19) ambaye wakala wake ni mchezaji wa
zamani wa Man United, Juan Sebastian Veron. Daily Mirror.
Burnley
wanaripotiwa kufanya mazungumzo na kiungo wa Swansea City, Jack Cork ambaye
anatarajiwa kujiunga na timu hiyo kwa dau la pauni milioni 10 (sh bilioni 29). Daily Mirror.

Newcastle
wameripotiwa kuhitaji huduma ya mshambuliaji wa Middlesbrough, Adama Traore
(21). Chronicle.

Crystal
Palace nao hawako nyuma kwenye usajili, kwani wako mbioni kumnyakua kiungo wa
Chelsea, Ruben Loftus-Cheek (21) kwa mkopo wa msimu mzima. Daily Telegraph
No comments