Header Ads

Jioni Njema; Man United wasafishiwa njia kwa Matic # Mbappe kuivunja ‘BBC’ Madrid # Leipzig wajiandaa kumuuza Keita



https://www.thesun.co.uk/wp-content/uploads/2017/07/nintchdbpict000338707287.jpg?strip=all&w=960&quality=100

MANCHESTER- MANCHESTER United imebaki peke yake kwenye mbio za kumsajili kiungo wa Chelsea, Nemanja Matic, baada ya wapinzani wao, Juventus kuelekeza nguvu zao kwa Blaise Matuidi wa PSG.
http://www.getfootballnewsfrance.com/assets/Mbappe-806x516.jpg
Mchambuzi wa soka Hispania, Guillem Balague amesema Real Madrid imevujisha siri kuwa, Kylian Mbappe atakua klabuni hapo iwapo mmoja wa wachezaji wanaounda kombinesheni maarufu BBC atauzwa. BBC ni Bale Gareth, Benzema Karim na Cristiano Ronaldo. Hata hivyo, Madrid imesema Mbappe anaweza kuja bila kubughudhiwa kwa BBC.
http://images1.minutemediacdn.com/production/912x516/58c7cefe3c43a26fae000001.jpg
Gazeti maarufu Ujerumani, Bild, limeripoti kuwa klabu ya RB Leipzig inajiandaa kimya kimya kuziba pengo la Naby Keita anayetarajiwa kuhamia Liverpool. Limeeleza kuwa Mkurugenzi wa Michezo, Ralf Rangnick amewatuma skauti watafute mbadala wa kiungo huyo.
http://i1.mirror.co.uk/incoming/article9930619.ece/ALTERNATES/s615/Liverpools-Philippe-Coutinho-celebrates-scoring-their-first-goal.jpg
Kwa mujibu wa mmoja wa watangazaji wa Radio Catalan ya mjini Barcelona, Gerard Romero, klabu ya mji huo, Barcelona tayari imekubaliana maslahi binafsi na Philippe Coutinho wa Liverpool na kilichobaki ni kukamilisha dili na Liverpool.
http://s2.asmonaco.com/img/article/79/2/9a8892/vadim-vasilyev-apporter-une-nouvelle-dynamique-1792_34.jpg
Makamu wa Rais wa Monaco, Vadim Vasilyev amesema wanafanya mazungumzo ya kuongeza mkataba na mshambuliaji wao, Kylian Mbappe. Pia kiongozi huyo amebainisha kuwa wachezaji wawili Thomas Lemar na Fabinho, hawaendi kokote licha ya kuhusishwa na kuondoka.
http://a.espncdn.com/combiner/i/?img=/media/motion/ESPNi/2017/0531/int_170531_Rumour_Rater_Perisic_to_Manchester_United/int_170531_Rumour_Rater_Perisic_to_Manchester_United.jpg&w=738&site=espnfc
Inter Milan imesema iko tayari kufanya biashara na Manchester United, kuhusu uhamisho wa Ivan Perisic. Bosi wa Inter, Luciano Spalletti amesema dili hilo lenye thamani ya pauni milioni 48 () litafanyika muda wowote. Sky Sports.



No comments

Powered by Blogger.