Header Ads

Marekani kuipa silaha Ukraine kupambana na waasi



Ukraine map - rebel-held territory

DONETSK- MJUMBE mpya wa Marekani nchini Ukriane, Kurt Volker amesema kuwa Marekani inatathmini ikiwa itatuma silaha kusaidia wale wanaopigana na waasi wanoungwa mkono na Urusi.
Volker aliiambia BBC kuwa, kuihami serikali ya Ukraine itabadilisha msimamo wa Urusi. Alisema hafikirii kuwa hatua hiyo itakuwa ni uchokozi.
Wiki iliyopita Wizara ya Mashauri ya Nje ya Marekani, ilizitaka pande zote mbili kusitisha mapigano Mashariki mwa Ukraine.
“Silaha za kujilinda, zile ambazo zitaisaidia Ukraine kujilinda na kuharibu vifaru kwa mafano, ambazo zitaizuia Urusi kuitisha Ukraine,” Volker aliiambia BBC.
Alisema kuwa, mafanikio ya kuwepo amani Mashariki mwa Ukraine yanahitaji kile alichokitaja mchakato wa mazungumzo na Urusi. Volker na mjumbe wa zamani wa Marekani kwenye NATO, na aliteuliwa kwenye wadhifa huo mpya mwezi huu.
Umoja wa Mataifa (UN), umesema kuwa zaidi ya watu 10,000 wameuawa tangu mzozo wa Mashariki mwa Ukraine uanze mnamo April, 2014 mara baada ya Urusi kulimega eneo la Crimea.  Mapigano hayo yamesababisha zaidi ya watu milioni 1.6 kuhama makwao.

No comments

Powered by Blogger.