Justin Bieber afuta matamasha yake yote
LOS ANGELES-
MWANAMUZIKI wa mtindo wa Pop, Justine Bieber amefutilia mbali safari yake ya
kikazi katika miji iliyotajwa kufanyka mjini hapa bila kutoa sababau yoyote ya
kufikia maamuzi hayo
Tamasha lililofutwa,
litaathiri ratiba ya matamasha ambayo yangefanyika Amerika ya Kaskazini na Asia
na ianelezwa wazi kwamba, gharama za kiingilio zitarejeshwa kwa mashabiki wake.
Taarifa
iliyotolewa na uongozi wa masanii huyo, inasema Bieber anawapenda mashabiki
wake na hapendi kuwakwaza na akatumia fursa hiyo kutoa shukrani zake kutokana
na uhusiano mzuri ambao umekuwapo baina yake, uongozi na wasaidizi wake kwenye
matamasha zaidi ya 150 katika mabara 6 tofauti.
Hatua hiyo,
inakuja baada ya kutafakari kwa kina msanii huyo nyota wa pop ameamua hataimba
tena kwenye matamasha yaliyosalia, Bieber mwenye miaka 23 hajatoa kauli yoyote
wala kuandika chochote kwenye kurasa zake za mitandao ya kijamii
Mtandao wa
celebrity news ulikinukuu chanzo kimoja na kuarifu kuwa, mwanamuziki huyo raia
wa Canada amefutilia mbali matamasha yaliyo salia bila sababu za msingi
Mwishoni mwa
wiki iliyopita, msanii huyo alipigwa picha akitembea mlimani na mjini hapa
akiwa na na binti mdogo ambaye walionekana kuwa na mahusiano mazuri
Bieber
alianza msururu huu wa matamasha kwa nguvu kubwa ya albamu yake ya ‘Purpose’
aliyoitoa Machi 2016, na tayari ametumbuiza matamasha zaidi ya 150 kwenye bara
la Ulaya, Afrika, Amerika ya Kusini, Australia na maeneo ya bara Asia
Hatua hiyo
ya Bieber, inakuja siku kadhaa baada ya msanii huyo kukatazwa kufanya matamasha
nchini China sababu ya tabia mbaya kama ilivyoarifiwa na mamlaka mjini Beijing
Licha ya
kusifia mapenzi waliyo nayo mashabiki kwa msanii huyo, lakini mamlaka hizo
hazikuweka wazi ni tabia zipi za kukera alizozionesha msanii huyo kiasi cha
kukatazwa kufanya matamasha nchini humo
Bieber tangu
alipoanza muziki, amekuwa kama mwizi wa mioyo ya mashabiki wake kwa mapenzi
makubwa waliyo nayo kwake na kazi zake.
BBC
No comments