Buhari kurejea Nigeria wiki mbili zijazo
LONDON- GAVANA
wa jimbo la Imo nchini Nigeria, Rocha Okorocha amesema kuwa anatarajia Rais
Muhammadu Buhari kurudi nyumbani kutoka Uingereza katika kipindi cha wiki mbili
zijazo.
Gavana Okorocha
alikuwa mmoja wa ujumbe uliokutana na rais huyo mwishoni mwa wiki iliyopita. Buhari
amekuwa akipata matibabu nchini, kwa ugonjwa ambao haujawekwa wazi.
Kutokuwepo
kwake kumezua hali ya wasiwasi nchini Nigeria, huku watu wakidai kwamba huenda
amefariki. Wengine wamekuwa na wasiwasi kwamba huenda asirudi tena.
Baadaye Ikulu
ilitoa picha za Buhari mwenye umri wa miaka 74, akikutana na magavana kutoka chama
chake. Ni mara ya kwanza amepigwa picha mjini hapa, tangu aondoke Nigeria
yapata siku 80 zilizopita.
Gavana Okorocha
aliiambia BBC jana kwamba; “Nilikutana na mtu mwenye motisha na anendelea vema.
Hajapoteza ucheshi wake kama anavyojulikana.
Kwa hivyo
anaendelea vyema na tunafurahi kumuona, na tunadhani amefanya kitu muhimu
kuwahakikishia raia wa Nigeria kuhusu afya ya rais wao.”
Awali, Okorocha
alisema kwamba, Buhari alipuuzilia mbali uvumi kuhusu afya yake alipoulizwa.
BBC
No comments