Baba wa bibi harusi apigwa na radi harusini Canada

NEW
BRUNSWICK- HAKUNA mtu anayependa kuona harusi ikiharibika, lakini baba mmoja
ameshikwa na hofu kutokana na kilichotokea wakati wa harusi ya binntiye.
JP Nadeau
anaripotiwa kupigwa na radi wakati akitoa hotuba huko New Brunswick, Canada.
“Wakati nilipokuwa
nikimwambia mkwe wangu, ‘Una bahati sana’- ndipo kuliposikika kitu kama bomu,”
alikimbia kituo kimoja cha habari nchini hapa.
Kando na
jeraha alilopata kwenye kidole chake, Nadeau hakuhofu na sherehe hiyo ya harusi
iliendelea. Kila mtu alishangazwa kwanza, lakini hilo halikusababisha sherehe
kusitishwa.
“Ilikuwa
harusi nzuri na iliyofana,” mke wake Nadeau alikiambia kituo cha CBC.
Nadeau amesema
kuwa, yeye ni mtu mwenye bahati kwa sababu mwaka 2015 meli aliyokuwa akifanya
kazi ilishika moto karibu na visiwa vya Falkland, lakini aliokolewa na Jeshi la
Anga la Uingereza.
No comments