Makaburi ya watu wenye vipara yafukuliwa Msumbiji
Katika
siku za karibuni, kumezuka imani potofu ambapo baadhi ya watu wanaamini kwamba kichwa
cha mtu mwenye kipara kina dhahabu. Tukio hilo la kufukuliwa kwa makaburi hayo,
limesababisha wakazi wa Milange kuiomba Serikali kuingilia kati na kuimarisha
ulinzi.
Mwezi
uliopita, kamanda mmoja wa polisi aitwaye, Afonso Dias, aliiambia kuwa misururu
ya mauaji ya watu wenye vipara imekuwa ikisababishwa na imani hizo potofu.
Kufikia
sasa wakaazi, na watumiaji wa dawa za kitamaduni pamoja na waliopigania uhuru
wamekutana na maofisa wa taasisi ya kitaifa ya urithi na usaidizi wa haki (IPAJ).
Mwakilishi
wa IPAJ, Antonio Gussi aliahidi kuwasilisha malalamishi yao kwa mamlaka husika,
lakini pia akawataka kutokubali tamaduni hizo zilizopitwa na wakati katika siku
za usoni.
BBC
No comments