Header Ads

Maji ya Mto Msimbazi hayafai

https://blogger.googleusercontent.com/img/b/R29vZ2xl/AVvXsEg23-7xR9Dxyl1VwFOzx9xhMGf9GL0fggUNVdSxHSSMuLQS7GXMv_v8ma_YGX4H0uWgRN4wxCql8u3_C02qJz0fkEay1VMmU2VBa-oTAtylUVk_oc7BrxK2R4qlyFVgs9AeK1KIxzW9hraO/s1600/5.jpg


DAR ES SALAAM- SERIKALI imechukua sampuli ya maji ya Mto Msimbazi kwa ajili ya kuyachunguza, ili kubaini kiwango cha sumu na ubora wa maji yake kwa matumizi ya binadamu.

Akitoa matokeo ya awali kwa wanahabari, Meneja wa Maabara ya Mazingira wa Ofisi ya Mkemia Mkuu, Emanuel Gwae, amesema kipimo cha maji ya Mto Msimbazi, katika eneo la Jangwani, kinaonyesha maji hayo yana kiwango cha oksijeni cha milimita 3.3.
Amesema kiwango hicho ni kidogo na kwamba kinachohitajika ni kuanzia milimita sita.
“Hii inaonyesha namna ambavyo maji haya yamechafuka na viumbe hai waliomo humu hawawezi kuishi,” amesema Gwae.
Mchakato wa upimaji wa maji hayo umefanyika leo, Jumanne, Julai 11 katika tukio ambalo Naibu Waziri wa Nchi, Ofisi ya Makamu wa Rais Muungano na Mazingira, Luhaga Mpina alilishuhudia.
Katika hatua nyingine, Ofisi ya Mkemia Mkuu ilichukua sampuli hiyo ya maji ambapo Waziri Mpina alishiriki kuchota maji hayo kwa ajili ya kupimwa.
Mbali na ofisi ya Mkemia Mkuu wa Serikali, wadau wengine waliokuwepo ni pamoja na Shirika la Viwango Tanzania (TBS) Bonde la Wami-Ruvu na Baraza la Usimamizi na Uhifadhi wa Mazingira (NEMC).
Chanzo; Mwananchi


No comments

Powered by Blogger.