Header Ads

Carrick akabidhiwa unahodha Man United huku Januzaj akipigwa bei



http://www.manutd.com/sitecore/shell/~/media/E03629C0727F458C9A6A7AD6A40ECBBE.ashx?w=1280&h=720&rgn=0,66,2480,1462

LOS ANGELES- KLABU ya Manchester United imemchagua kiungo wake wa kati, Michael Carrick kuwa nahodha wa klabu hiyo.
Carrick (35) kwa sasa ndiye mchezaji aliyeichezea Man United kwa kipindi kirefu, baada ya kujiunga na United 2006 na anachukua nafasi ya Wayne Rooney ambaye amehamia klabu ya Everton.
“Nahisi ni fursa kubwa kuiongoza uwanjani timu kama Manchester United. Sikudhani kwamba, nitasalia katika klabu hii kwa muda huu mrefu na kufanikiwa hivi .Nimekuwa nikiipenda klabu hii na kuwa katika nafasi hii ni kitu maalum kwangu,” Carrick aliiambia MUTV.
http://e0.365dm.com/16/01/16-9/20/adnan-januzaj-manchester-united-u21s-januzaj-in-action_3402203.jpg?20160118222605
Kwa upande mwingine, klabu hiyo imekubali kumuuza mshambuliaji wao, Adnan Januzaj (22) kwa Real Sociedad ya Hispania, kwa dau la pauni milioni 9.8 (sh bilioni 284) baada ya mchezaji huyo kushindwa kupata nafasi kwenye kikosi cha kwanza cha United.



No comments

Powered by Blogger.