Header Ads

Lipumba: Maalim Seif ndiye kawaponza wabunge waliofukuzwa CUF



http://www.eatv.tv/sites/default/files/styles/detailpageimg/public/news/2017/07/27/CUF.jpg?itok=rApcTFKa&timestamp=1501149154

DAR ES SALAAM- MWENYEKITI wa (CUF) anayetambuliwa na Ofisi ya Msajili wa Vyama vya Siasa, Profesa Ibrahim Lipumba amesema wabunge nane wa chama hicho waliovuliwa uanachama wameponzwa na Katibu Mkuu wa CUF, Maalim Seif Sharif Hamad.
Profesa Lipumba ameyasema hayo leo, alipokuwa akizungumza na waandishi wa habari na kusema Maalim Seif na yeye ana yake ya kujibu mbele za Kamati ya Maadili na Nidhamu ya chama hicho. 
“Katibu Mkuu, Naibu Katibu Mkuu na kuna wananchama wengine wengi tu ambao pia wana makosa ya kuweza kujibu mbele ya Kamati ya Nidhamu na Maadili. Katika watu wote hao, Katibu Mkuu yumo na yeye ndiye amewaponza hawa wabunge nane wa Viti Maalum ambao wamevuliwa uanachama,”
“Wale wabunge wengine, wala msiwe mnasikiliza na kufuata kila anachosema Katibu Mkuu atawaponza kama alivyowaponza wajumbe wa Baraza la Wawakilishi,” alisema Lipumba. 
Kwa upande wa Katibu Mkuu wa CUF Taifa, Maalim Seif Sharif Hamad amesema mpaka sasa wabunge wote nane ambao wanasemakama wamefukuzwa uanachama wameamua kufungua kesi Mahakama Kuu kupinga maamuzi feki ambayo yamefanywa na Baraza Kuu feki.
Aidha, Maalim Seif aliiitaka Mahakama itamke kuwa hao ni wanachama halali wa CUF na wabunge halali wa Bunge la Jamhuri ya Muungano wa Tanzania.
“Baraza Kuu halali la CUF litakutana kwa dharura kesho Ijumaa Julai 28, ili kujadili mambo mbalimbali ambayo yanaendelea katika chama hicho na kutangaza hatua ambazo zitafuata,” alisema Maalim Seif. 
Chanzo; EATV

No comments

Powered by Blogger.