Israel yaondoa hatua zote za kiusalama Jerusalem

TEL AVIV-
SERIKALI imeamua kuondoa hatua zote za kiusalama, ambazo zilikuwa zimewekwa
ndani ya eneo lote takatifu la Msikiti wa Al Aqsa jijini Jerusalem.
Kwa mujibu
wa taarifa ya polisi, hatua hizo zimeondolewa ili kusitisha maandamano ya
Wapalestina ambao walikuwa wakipinga hatua hiyo ya Serikali.
Mara baada
ya kuondolewa kwa hatua hiz, viongozi wa dini katika utawala wa Palestina walisema
kwa sasa wataacha kususia eneo hilo takatifu.
Vizuizi
hivyo viliendelelea leo asubuhi, siku mbili baada ya mitambo ya kutambua chuma
kuondolewa. Vifaa hivyo viliwekwa, baada ya tukio la kuuawa kwa polisi wawili
wa Israel katika eneo hilo na mtu ambaye aliingia na silaha.
Israel
imesema kuwa itachukua hatua zisizokuwa na vizuizi miezi sita inayokuja.
Kumekuwa na
karibu makabiliano ya kila siku kati ya vikosi vya usalama vya Israel na
waandamanaji, tangu mitambo ya kutambua chuma iwekwe baada ya kuuwawa kwa
polisi Julai 14 mwezi huu karibu na eneo linalofahamika kama Haram al-Sharif
kwa Waislamu na Temple Mount kwa Wayahudi.
Wapalestina
wanne waliuawa na raia watatu wa Israel kuuliwa, kwa kuchomwa visu na Mpalestina
ambaye alidai alikuwa akilipiza hatua za Israel eneo takatifu.
BBC
No comments