Korea Kaskazini yafanya jaribio tena
![https://ichef-1.bbci.co.uk/news/660/cpsprodpb/C2C5/production/_97116894_northkorea1.jpg](https://ichef-1.bbci.co.uk/news/660/cpsprodpb/C2C5/production/_97116894_northkorea1.jpg)
SEOUL- MOAFISA wa Serikali nchini pamoja na Japan,
wamesema Korea Kaskazini imefanya jaribio jingine la kombora ambalo limeonekana
likianguka katika eneo la bahari karibu na Japan.
Jaribio hilo
linakuja katika kipindi ambacho, Marekani ilitoa onyo kuwa taifa hilo linaweza
likafanya jaribio muda wowote na tayari imetangaza kuiwekea Korea Kaskazini vikwazo
vipya.
Kombora hilo
lilirushwa kutoka mkoa wa Jagang, ulio Kaskazini mwa taifa hilo, kulingana na
chombo cha habari Yonhap.
Katibu wa Baraza
la Mawaziri nchini Japan, Yoshihide Suga alisema kuwa kombora hilo lilisafiri
kwa takriban dakika 45 ikilinganishwa na kombora la masafa marefu lililofanyiwa
majaribio mwanzoni mwa Julai mwaka huu.
Anasema kuwa
lilianguka katika bahari ya Japan, lakini siyo katika maji ya himaya ya Japan.
Kulingana na
taarifa ya Yonhap, Rais Moon Jae-in alilazimika kuitisha mkutano wa kiusalama usiku
wa kuamkia leo.
Mapema Julai
mwaka huu, Korea Kaskazini ilidai kufanikiwa kulifanyia jaribio kombora la
masafa marefu kwa mara ya kwanza. Kombora hilo ni la hivi karibuni, katika
msururu wa makombora yaliyofanyiwa majaribio hatua inayokiuka marufuku ya UN.
Umbali wa
kombora hilo haujulikani licha ya kupingwa, lakini wataalam wanasema kuwa
linaweza kufika Alaska nchini Marekani.
Msemaji wa
Pentagon, Jeff Davis alisema kuwa kombora hilo lilirushwa na kwamba habari
zaidi zinasubiriwa. Kombora hilo la hivi karibuni ni la 14 kurushwa na Korea
Kaskazini kwa mwaka 2017.
BBC.
No comments