Header Ads

Takukuru yawakamata wagombea wa TFF



http://www.eatv.tv/sites/default/files/styles/detailpageimg/public/news/2017/07/26/takukuru.jpg?itok=zo_qfTPU&timestamp=1501081665

MWANZA- BAADHI ya wagombea wa nafasi mbalimbali za uchaguzi za Shirikisho la Mpira wa Miguu Tanzania (TFF) na wadau wa soka, wamekamatwa na Taasisi ya Kupambana na Kuzuia Rushwa (TAKUKURU) kwa tuhuma za kujihusisha na rushwa jijini hapa.
Akizungumza kuhusu kukamatwa kwa watu hao, Msemaji wa Takukuru, Ernest Makale alisema watu hao walikamatwa baada ya kufuatiliwa nyendo zao na kubaini dalili za uwepo wa rushwa.
Makale aliwataja waliokamatwa kuwa ni, Mwenyekiti wa Chama cha Soka Dar es Salaam (DRFA), Almas Kasongo, Shafii Dauda, Elias Mwanjale, Leonald Malongo, Effam Majinge, Osuri Kasuli, Richard Kayenzi, Lazack Juma pamoja na Kelvin Shevi.
“Tumewakamata, kwa sababu hiki siyo kipindi cha kampeni na dalili zote kwamba walikuwa hapa kwa ajili ya uchaguzi unaotarajiwa zilikuwa zipo wazi,”
“Kama Takukuru tumeona kuwa, kuna viashiria vya rushwa na ndipo tukaweka mitego yetu kwenye sehemu walizokuwa wanaendeshea vikao vyao vya siri ndipo tulipoweza kuwakamata,” alisema Makale.

Pamoja na hayo, Makale alisema watuhumiwa hao waliachiwa kwa dhamana ila wanaendelea na uchunguzi wao endapo watakapopata ushahidi wa kutosha watafikishwa mahakamani.
Chanzo; EATV

No comments

Powered by Blogger.