Header Ads

Jaribio la kifaa cha kuwalinda wanawake dhidi ya Ukimwi lafanikiwa




Watafiti nchini Marekani wanasema kuwa jaribio ambalo vijana wa Marekani walitumia mviringo kujilinda na virusi vya HIV limefanikiwa.

PARIS- WATAFITI nchini Marekani, wamesema kuwa jaribio ambalo vijana wa Marekani walitumia mpira wa mviringo kujilinda na virusi vya Ukimwi (VVU) limefanikiwa.
Utafiti zaidi sasa utafanywa kwa vijana barani Afrika. Katika utafiti huo, wasichana walitumia mviringo wa plastiki uliowekwa dawa za kujilinda na Ukimwi, ambao ulibadilishwa kila mwezi baada ya kipindi cha miezi sita.
Ni mojawapo ya mipango ya kutengeza kifaa ambacho, wanawake watatumia kujilinda dhidi ya maambukizi ya VVU ili wasiweze kuwategemea wanaume kuvaa mipira ya kondomu.
Wakiripoti ugunduzi huo mpya kuhusu virusi vya VVU mjini hapa, watafiti hao walisema wanafurahi kwamba wasichana hao walitumia kifaa hicho na kusema kuwa wamekipenda.
Wanawake na wasichana walio na kati ya umri wa miaka 15-24, wanadaiwa kuwa moja kwa tano ya visa vyote vya maambukizi ya HIV duniani.
Takriban wanawake 1,000 huambukizwa virusi kila siku katika bara la Afrika hususan katika mataifa ya Kusini mwa Jangwa la Sahara.
BBC.

No comments

Powered by Blogger.