Header Ads

Mezani Jioni; Monaco haijamuuza Mbappe # Liverpool yamrudia Keita # Neymar kuondoka Barca



http://i2.mirror.co.uk/incoming/article10058710.ece/ALTERNATES/s615/Monacos-French-forward-Kylian-Mbappe-Lo.jpg

MADRID- MONACO imeiambia Sky Sports kwamba, hawajakubaliana kwa namna yoyote na Real Madrid kuhusiana na dili la kumsajili Kylian Mbappe (18) na kukanusha uvumi kuwa wamekubaliana kiasi cha pauni milioni 160 (sh bilioni 464). Sky Sports.
http://images.performgroup.com/di/library/GOAL/34/ed/neymar-las-palmas-barcelona-laliga-14052017_16fvmujdpw9f01ocako3c3ggt7.jpg?t=143666796&w=620&h=430
Hatima ya mshambuliaji wa Barcelona na Brazil, Neymar (25) iko shakani, kutokana na vyanzo vya karibu na mchezaji huyo kudai kuwa mchezaji huyo ataenda PSG. Vyanzo hivyo vinadai kuwa, kuna uwezekano wa asilimia 90, Neymar kuhama kukimbia kivuli cha Lionel Messi. Sky Sports.
https://static.independent.co.uk/s3fs-public/styles/story_medium/public/thumbnails/image/2017/07/21/11/naby-keita.jpg
Kwa mara nyingine tena, Liverpool imewasilisha dau la pauni milioni 74 (214.6), mezani kwa klabu ya RB Leipzig, kwa ajili ya kumsajili kiungo mahiri wa timu hiyo, Naby Keita (22) baada ya kukataliwa mara mbili awali. Daily Star.
https://www.thesun.co.uk/wp-content/uploads/2017/05/nintchdbpict000325669740-e1495467930364.jpg?strip=all&w=960&quality=100
Barcelona wanatarajiwa kuwasilisha ofa ya pili kwa Liverpool, ili kuruhusiwa kumnunua kiungo mahiri, Philippe Coutinho (25) baada ya ofa yao ya kwanza ya pauni milioni 72 (sh bilioni 208.8) kukataliwa. Hata hivyo, bosi wa Liverpool, Jurgen Klopp amesema mchezaji huyo hauzwi. Sky Sports.
https://blogger.googleusercontent.com/img/b/R29vZ2xl/AVvXsEgzgZZy6Xm1tigZzjYkCWntNlVaiZ8dN3E5lRyCPaiNkaXz83zgsuTfoMstVPYxrsV6UnTn_sbOTpyjp3pDd-QKI2Ek2pTkXYz0p_t2jg29xV7N-9XOHp2F684MDxSRaI7S2BZ2qO_e1Nkt/s1600/ScreenShot027.jpg
Baada ya kushindwa kumsajili Fabinho kutoka Monaco, matajiri wa Paris, PSG wameelekeza fedha zao kwa kiungo wa Porto ya Ureno, Danilo Pereira (25). Hata hivyo, Porto wana uhakika wa kuingiza pauni milioni 60 (sh bilioni 174) kama ada ya kumuuza mchezaji huyo. Le10Sport.
http://a.espncdn.com/combiner/i/?img=/photo/2015/0130/soc_g_lamela_d1_1296x729.jpg&w=738&site=espnfc
Inter Milan inaripotiwa kuandaa dau la pauni milioni 15 (sh bilionii 43.5), kwa ajili ya kumsajili winga wa Tottenham Hotspurs, Erik Lamela (25) lakini Spurs wanataka pauni milioni 18 (sh bilioni 52.2). Sky Sports.
http://i4.mirror.co.uk/incoming/article7760637.ece/ALTERNATES/s1200/Player-of-the-Year-nominee-Riyad-Mahrez.jpg
Riyad Mahrez anaendelea kufanya mazoezi na wenzake kama ilivyo kawaida, licha ya kuwepo kwa taarifa kuwa Roma imewasilisha dau lililoboreshwa na kufikia pauni milioni 30 (sh bilioni 87), baada ya dau la kwanza kukataliwa. Sky Sports.

No comments

Powered by Blogger.