Header Ads

Lisu: Tutaendelea kumkosoa JPM

http://www.thecitizen.co.tz/image/view/-/3946870/medRes/1655755/-/9w8hcrz/-/pic+lissu.jpg?format=xhtml

DAR ES SALAAM- SAA chache baada ya kuachiwa kwa dhamana huku akiwa amesota rumande kwa siku saba, Mwanasheria Mkuu wa Chadema ambaye pia ni Rais wa Chama cha Wanasheria Tanganyika (TLS), Tundu Lissu amesema wapinzani wataendelea kuzungumza na kumkosoa Rais John Magufuli.

Akisisitiza kuwa kifo ndiyo njia pekee ya kuzuia hilo lisitokee, amesema: "Wanataka tunyamaze ili waendeshe nchi hii wanavyotaka wao. Taifa hili ni la mfumo wa vyama vingi, tuna haki ya kufanya mikutano, tuna haki ya kufanya maandamano na tuna haki ya kutoa maoni yetu.

“Kwa msingi huo hakuna wa kutunyamazisha nchi hii si mali ya mtu binafsi.

Alisema hayo jana katika mkutano wake na wanahabari, muda mfupi baada ya kupewa dhamana akibainisha kuwa kukamatwa na kuwekwa mahabusu na hata kufungwa, hakutamzuia kusema na kumkosoa Rais kwani akiwekwa mahabusu au kufungwa, atazungumza akiwa kifungoni.

"Ukisema tu unakumbana na Segerea ili tumwachie yeye peke yake, hatutamwachia. Hakuna gereza litakalotunyamazisha … atupeleke mahabusu kwa sababu tutazungumza tukiwa huko, hata akitufunga tutasema tukiwa kifungoni,” alisema.

"Njia rahisi ya kwenda mbinguni ni kupinga uonevu, itabidi tufe kwanza ili tusiseme, mwambieni Magufuli tutanyamaza tukiwa wafu kwa sababu wafu hawasemi".

Alibainisha kuwa kunyamaza kunaweza kusababisha nchi kuangamia, na kwamba hakuna atakayewanyamazisha.

No comments

Powered by Blogger.