Header Ads

Gari lenye bango la kampeni za Joho lakamatwa operesheni dawa za kulevya Mombasa



http://www.the-star.co.ke/sites/default/files/styles/new_full_content/public/1604013.jpg?itok=xQQ4olyA

MOMBASA- POLISI wa Kitengo cha Kupambana na Dawa za Kulevya mjini hapa, wanashikilia gari yenye mabango ya kampeni ya Gavana wa Mombasa, Hassan Joho ambayo ilikamatwa katika mtaa wa Nyali ikihusishwa na dawa hizo.
Mkuu wa Polisi mjini hapa, Larry Kieng alisema gaari hilo lilikamatwa kwenye msako maalum pamoja na watuhumiwa watatu wa dawa za kulevya waliokuwa wakitafutwa kwa muda mrefu wakiwa na dawa zenye thamani ya mamilioni ya shilingi.
Aidha, wapelelezi hao wa polisi walifanikiwa kukamata kiasi cha fedha cha shilingi milioni 4.5 za Kenya na dola za Marekani 10,000 ambazo zinaaminika zilikuwa zikitumika kwenye uagizaji na usambazaji wa dawa hizo.
“Ni kweli tumelikamata gari hilo lenye mabango hayo, ambayo yanamnadi Joho. Lakini hatutaweza kusema kwa sasa kuwa gari hilo ni lake, hadi hapo tutakapopata vithibitisho kutoka kwa Mamlaka ya Mapato Kenya (KRA) kwani tumewasiliana nao,” alisema Kieng.
Kieng alisema watuhumiwa hao walitambuliwa kuwa ni Abdullahi Ahmad Kheri (raia wa Tanzania), Hope Mbaga na Musa Kihara ambao wote ni Wakenya.
Gari hilo lilikuwa lilikamatwa likiwa limesihifadhiwa kwenye yadi ya moja ya majengo yanayomilikiwa na watuhumiwa hao.
The Star.

No comments

Powered by Blogger.