Header Ads

Breaking; Lissu apata dhamana atakiwa kutotoka nje ya Dar es Salaam



IMG-20170724-WA0008.jpg

DAR ES SALAAM- MAHAKAMA ya Hakimu Mkazi Kisutu imemuachia leo asubuhi kwa dhamana ya Shilingi milioni 10 Rais wa Chama cha Wanasheria Tanzania (TLS) na Mwanasheria Mkuu wa Chadema, Tundu Lissu.
Aidha, Mahakama hiyo imemuamuru Lissu ambaye ni mbunge wa Singida Mashariki, kutotoka nje ya Dar es Salaam kama moja ya masharti ya dhamana hiyo ya kesi hiyo.
Dhamana hiyo inakuja kufuatia ombi la mawakili wa Serikali, la kuiomba mahakama imnyime Lissu dhamana kutupiliwa mbali na Hakimu Mkazi, Wilbard Mashauri.
Julai 24, Mbunge huyo alinyimwa dhamana na kutakiwa abaki rumande hadi leo ambapo Mahakama itatoa uamuzi wa dhamana, kutokana na upande wa Jamhuri kuwasilisha pingamizi. 
Mahakama hiyo ilifikia uamuzi huo, baada ya mawakili wa Lissu, Fatma na wa Serikali, Mutalemwa Kishenyi na Saimon Wankyo kujibizana kwa hoja kwa zaidi ya saa mbili.
Baada ya majibizano hayo, Hakimu Mkazi Wilbard Mashauri aliahirisha kesi hiyo hadi leo ili apitie hoja hizo na kuziandikia uamuzi na ndipo alipoamua kumuachia kwa dhamana.



No comments

Powered by Blogger.