Kiongozi wa waasi ajisamilisha DR Congo
Kikosi
maalumu cha kulinda amani nchini, (MONUSCO), kimesema Sheka ndiye kiongozi mkuu
wa kijeshi wa kundi lililokuwa likijulikana kama Mai-Mai Sheka, ambaye aliamua
kujisalimisha karibu na ngome yake Mashariki mwa nchi.
Baada
ya kujisalimisha, hatua inayofuata ni kukabidhiwa kwa Serikali ya nchi, ambayo
miaka sita iliyopita ilitoa hati ya kukamatwa kwake kwa madai na makosa ya
Uhalifu dhidi ya Binadamu na Uhalifu wa vita.
Kundi
hilo la Mai-Mai Sheka, linatuhumiwa pia kwa makosa ya ubakaji na ukatili wa
kutisha wa kuwatesa raia na na kuwaacha wafe taratibu.
Shirika
la Kutetea Haki za Binadamu lililoko mjini New York, limetoa rai kwa Serikali kumtendea
mtuhumiwa huyo ubinadamu wakati wote wa kesi yake na kwamba haki zake kama binadamu
zisikiukwe.
BBC

No comments