Header Ads

Ikulu ya Marekani yadai azimio la kumng’oa Trump halina maana


PHOTO: Rep. Al Green (D-TX), accompanied by Rep. Brad Sherman (D-CA), speaks with the media about his plans to draft articles of impeachment against President Donald Trump on Capitol Hill in Washington, June 7, 2017.
Wabunge wawili wa chama Democratic, Al Green wa D-Texas na Brad Sherman wa D-California ambao wamewasilisha azimio la kulitaka bunge la Congress kumuondoa madarakani Rais Donald Trump.

WASHINGTON DC- IKULU ya Marekani, imesema azimio la kulitaka bunge kumuondoa madarakani Rais, Donald Trump, ambalo limewasilishwa na wabunge wawili wa Congress kutoka chama cha Democratic, halina maana.
Azimio hilo liliwasilishwa jana bungeni hapo na wabunge wawili ambao ni, Al Green kutoka D-Texas na Brad Sherman kutoka D-California. Kwa pamoja, wabunge hao wanataka bunge kutumia sheria iliyopitishwa mwaka 1974 inayohusiana na kizuizi cha haki, ambao ulitumika kumuondoa Rais Richard Nixon.
Msemaji wa Ikulu, Sarah Huckabee Sanders alisema azimio hilo linadai kwamba Trump alitumia mamlaka yake kuzuia uchunguzi na kusababisha kusitishwa kwa uchunguzi wa madai ya Urusi kuingilia uchaguzi wa mwaka jana.
“Nafikiri kwa ujumla azimio hilo halina maana kabisa na ni mchezo wa kisiasa ulio kwenye ubora wake mbaya,” Huckabee alisema wakati alipokuwa akizungumza na waandishi wa habari bila kuongeza maoni mengine.
abc NEWS


No comments

Powered by Blogger.