Header Ads

Marekani kuziwekea vikwazo Urusi, Iran na Korea Kaskazini



Putin na Trump kwa pamoja wamekana Urusi kuingilia uchaguzi wa Marekani

WASHINGTON DC- BARAZA la Wawakilishi la Marekani (Congress), limepiga kura ya kuidhinisha kuwekwa kwa vikwazo vipya dhidi ya Urusi, Iran na Korea Kaskazini.
Urusi inaadhibiwa kutokana na kudaiwa kuingilia uchaguzi mkuu wa mwaka jana nchini, huku Korea Kaskazini na Iran wao wakiadhibiwa kufuatia majaribio ya makombora.
Muswada huo unatarajiwa kupitia kwa Baraza la Seneti, kabla ya kupelekwa kwa Rais Trump ili auidhinishe na kuwa sheria kamili.
Akizungumza katika baraza hilo, David Ciciline kutoka chama cha Democratic, alisema hatua kamili zinahitajika kuiwajibisha Urusi.
Ciciline alisema hawawezi kuruhusu dola nyingine kuingilia uchaguzi wao japokuwa Rais wao anapinga kuihusisha Urusi na uchaguzi uliopita.
Naye Ted Poe kutoka chama cha Republican, alisisitiza kuwa muswada huo unaihusisha Korea Kaskazini pia.
Mwenyekiti wa kamati ya mahusiano ya kimataifa ya Bunge la Urusi, (Duma), Leonid Slutsky alisema hatua hizo mpya zitazorotesha uhusiano baina ya Urusi na Marekani.
BBC.

No comments

Powered by Blogger.