Header Ads

Aishi bila kuwa na virusi vya Ukimwi licha ya kuzaliwa navyo



Image result for HIV

CAPE TOWN- WANASAYANSI nchini, wamebaini kwamba mtoto aliyeambukizwa Virusi Vya Ukimwi (VVU), amefanikiwa kuishi kwa miaka nane na nusu bila virusi hivyo.
Mtoto huyo, alipewa dawa za majaribio ya kukabiliana na virusi hivyo alipokuwa mdogo lakini hakuwahi kupewa tena dawa zozote za kukabiliana na VVU tangu afikishe umri wa mwaka mmoja.
Hii ni mara ya kwanza kwa mtu aliyekuwa na virusi hivyo kuweza kuishi bila virusi hivyo barani Afrika. Wanasayansi waliogundua kisa hicho, kwa sasa wanalinda utambuzi wa mtoto huyo ambaye ana umri wa miaka 9 na nusu.
Wanasema kuwa, visa kama hivyo ni vichache na kwamba familia ya mtoto hyo ina furaha. Dawa hiyo alipewa mtoto huyo wakati ambapo haikuwa suala la kawaida.
Watafiti wanaamini kupotea huko kwa vurusi siyo kwa sababu ya matibabu, lakini mtoto huyo ana jeni ama kinga isiyokuwa ya kawaida ambazo zimemlinda dhidi ya VVU.
BBC

No comments

Powered by Blogger.