Header Ads

Jioni Leo; Morata apewa namba 9 # Mendy atua Man City # City watumia £200 # Neymar aikoroga Barcelona



http://cdn.images.express.co.uk/img/dynamic/galleries/x701/266547.jpg

LONDON- CHELSEA imesema kuwa, mshambuliaji wao mpya kutoka Real Madrid, Alvaro Morata (24) atavaa jezi namba 9 wakati kipa wao, Willy Caballero atavaa namba 1 huku Antonio Rudiger akikabidhiwa namba 2 na kiungo Tiemoue Bakayoko atapatiwa namba 14. Sky Sports.
http://e1.365dm.com/17/07/16-9/20/skysports-benjamin-mendy-france_4000393.jpg?20170720171840
Beki wa kushoto wa zamani wa Monaco, Benjamin Mendy, amesaini mkataba wa miaka mitano wa kuichezea Manchester City kwa ada ya uhamisho ya pauni milioni 49.2 (sh bilioni 142.68) na kukabidhiwa jezi namba 22. Sky Sports.
https://s-media-cache-ak0.pinimg.com/originals/b8/4c/8a/b84c8a1e84185588913135e679c22d5f.jpg
Manchester City inakuwa klabu ya kwanza kwa Uingereza, kutumia zaidi ya pauni milioni 200 (sh bilioni 580) kwa msimu mmoja kufanya usajili na kuweka rekodi. Sky Sports.

http://a.espncdn.com/combiner/i/?img=/photo/2016/1027/r145768_1296x729_16-9.jpg&w=738&site=espnfc
Hatima ya mchezaji wa Brazil na Barcelona, Neymar, limeendelea kuikoroga Barcelona, baada ya jana mchezaji mwenzie, Gerald Pique kuposti kwamba mshambuliaji huyo haondoki lakini mtu wa karibu zaidi na Neymar amedai kuwa ataondoka. ESPN.
https://static.standard.co.uk/s3fs-public/thumbnails/image/2017/03/24/09/virgil-van-dijk-southampton.jpg
Southampton imeweka wazi orodha ya wachezaji walio kwenye kikosi chake kilichopo kwenye ziara za maandalizi ya kabla ya msimu, lakini kuna jina limekosekana nalo ni Virgil van Dijk. Klabu hiyo imedai kuwa, kwa sasa Dijk amekuwa akifanya mazoezi peke yake na anasisitiza anataka kuondoka klabuni hapo. Mail.
http://i2.mirror.co.uk/incoming/article10368505.ece/ALTERNATES/s615/Leicester-Citys-Riyad-Mahrez-celebrates-scoring-their-second-goal.jpg
Winga wa Leicester City, Riyad Mahrez (26) anaongoza orodha ya wachezaji wanaotakiwa kwa udi na uvumba na Roma ya Italia, licha ya kuwepo kwa tetesi kuwa miamba hiyo inamuwinda pia mchezaji wa Manchester City, Samir Nasri (30). Leicester Mercury.
http://e0.365dm.com/16/10/16-9/20/skysports-lucas-perez-arsenal-emirates-stadium_3818682.jpg?20161028111104
Mshambuliaji wa Arsenal, Lucas Perez (28), amepewa ofay a mkataba mnono wa miaka 10 na klabu ya Deportivo La Coruna, wakati kukiwa na sintofahamu kuhusu hatima ya Mhispania huyo pale Emirates Stadium. Metro.

No comments

Powered by Blogger.