Header Ads

Lissu anyimwa dhamana



IMG-20170724-WA0008.jpg

DAR ES SALAAM- MAHAKAMA ya Hakimu Mkazi Kisutu Dar es Salaam, imemnyima dhamana Mbunge wa Singida Mashariki na Mwanasheria Mkuu wa Chadema, Tundu Lissu, katika kesi ya uchochezi inayomkabili kiongozi huyo.
Aidha, kesi hiyo ambayo imesikilizwa kwa mara ya kwanza leo, imeahirishwa hadi Julai 27 mwaka huu.
Katika kesi hiyo, Lissu alikuwa akiwakilishwa na jopo la mawakili 21 wakiongozwa na Fatma Karume na Peter Kibatala huku upande wa Serikali ukiwakilishwa na mawakili watano.

No comments

Powered by Blogger.