Header Ads

Wataalam wagundua chanjo ya udukuzi



Watafiti wa usalama wamegundua chanjo ya shambulio la uhalifu wa mitandaoni lililoathiri mashirika tofauti duniani siku ya Jumanne.Image result for hackers
LONDON- WATAFITI wa usalama mitandaoni, wamegundua chanjo ya shambulio la uhalifu wa mitandaoni lililoathiri mashirika tofauti duniani jana.

Utengenezaji wa faili moja unaweza kuzuia shambulio la mashine yote. Hata hivyo, watafiti hao hawajafanikiwa kupata suluhu ya mara moja itakayoweza kuzuia kirusi hicho kuenea katika kompyuta nyingine ambazo hazina kinga.
Wataalam bado hawajui shambulio hilo linatoka wapi na lengo lake ni nini.
Huku ikidaiwa kwamba kikombozi inachotaka ni cha kiasi kidogo cha dola 300, wengi wanadai kwamba shambulio hilo linaweza kusababisha madhara mabaya zaidi ama hata kutoa tamko la kisiasa.
Image result for hackers
Baadhi ya waathiriwa wa shambulio hilo ni Benki Kuu ya Ukraine, kampuni kubwa ya mafuta kutoka Urusi, Rosnet, kampuni ya matangazo ya Uingereza, WPP na kampuni ya mawakili wa Marekani, DLA Piper.
Pia, waliopatikana katika shambulio hilo ni hospitali moja ya Marekani katika mji wa Pittsburgh. Lakini kwa wale walio na wasiwasi kuhusu shambulio hilo, kunaonekana kuna dawa inayoweza kudhibiti athari za kiini hicho.
Kwa kutengeza faili kwa jina Perfc na kuiweka katika "C:\Windows" folder, shambulio linaweza kusitishwa mara moja.  Maelezo ya kufanya hivyo yamechapishwa katika kompyuta ya usalama na kusaidiwa na wataalam wengine.
Hata hivyo, huku mbinu hiyo ikiwa ina uwezo wa kudhibiti kirusi hicho, ina uwezo wa kuzilinda kompyuta za kibinafsi ambazo faili zina Perfc. Watafiti kufikia sasa wameshindwa kupata suluhu ya kudumu itakayozuia shambulio hilo kabisa.
Ijapokuwa inaweza kuifanya mashine kuwa na kinga kama alivyoelezea mwanasayansi wa kompyuta, Profesa Alan Woodward, bado inaweza kusambaza kiini hicho katika kompyuta nyingine zilizounganishwa.
Kwa watumiaji wengi, kuweka Windows mpya ni suluhu ya kuzuia shambulio hilo iwapo ingetaka kuathiri komyuta yako.
Kusambaa kwa kirusi hicho kipya, kunaweza kuwa kwa mwendo wa pole ikilinganishwa na kile cha mwezi uliopita cha WannaCry na wataalam wametabiri huku wachangunuzi wa alama za siri wakisema kuwa kirusi hicho hakikuwa na lengo la kusambaa zaidi ya lengo lake.
Kutokana na hilo, wataalam kadhaa wanatabiri kwamba shambulio hilo halitasambaa sana kama lilivyofanya jana hadi pale kiini hicho kitakapoimarishwa.

No comments

Powered by Blogger.