Header Ads

Afa baada ya kumuokoa mwanae baharini



https://cbssanfran.files.wordpress.com/2017/06/brannan-island-drowning.jpg
RIO VISTA, California – MLINZI wa eneo la pwani mjini hapa, amesema mwanaume mmoja ambaye anakadiriwa kuwa na umri wa miaka 40, amepatikana akiwa amekufa baada ya kufanikiwa kumuokoa mwanae aliyezama baharini.

Imeelezwa kuwa mwanaume huyo ambaye ametambulika kama Roni Avila, alipotelea majini baada ya mwanae ambaye alikuwa ameambatana naye majini kwa boti maalum kuokolewa na ndege maalum ya uokoaji.
Awali kabla ya ndege hiyo kufika eneo hilo, Avila alikuwa amefanikiwa kumudu kumbeba bagani mwanae huyo mwenye umri wa miaka mitano baada ya kumuopa majini kutokana na mtoto huyo kuangukia majini.
Inadaiwa kuwa chombo hicho walichokuwa wakikitumia, kilipinduka na kusababisha mtoto huyo kuzama majini kabla ya kuokolewa na baba yake na kumbeba begani hadi hapo ndege hiyo ilipomwokoa na kisha yeye kuzama majini na kutoonekana hadi pale mwili wake ulipoonekana.
Kwa mujibu wa wachunguzi maalum na walinzi wa pwani, Avila na mwanae huyo wa kike hawakuwa wamevaa maboya kwa ajili ya kuwanusuru kwenye kadhia za kuzama baharini.

No comments

Powered by Blogger.