Header Ads

Kupanda kwa bei kukwamisha usajili wa Morata Man United



Image result for Alvaro Morata in his honeymoon
MANCHESTER- MPANGO wa klabu ya Manchester United kumsajili mshambuliaji wa Real Madrid, Alvaro Morata, huenda ukakwama kutokana na kupanda kwa bei ya mchezaji huyo.

Kwa mujibu wa gazeti la Mirror, bei ya Morata imepanda hadi kufikia pauni milioni 80 (sh bilioni 176) ikiwa ni ziada ya pauni milioni 8 kutoka ile ya awali ya pauni milioni 72.
Hata hivyo, vyombo vingi vimeripoti kwamba mchezaji huyo mwenye umri wa miaka 24 amekatisha fungate yake ili aweze kuharakisha uhamisho wake kuelekea Man United.

No comments

Powered by Blogger.