Pacquiao mbioni kuzichapa na Mayweather tena
BRISBANE-
LEGENDARI wa ngumi wa Kifilipino, Manny Pacquiao anakaribia kutimiza ndoto zake
za kurudiana tena na Mmarekani, Floyd Mayweather, iwapo tu atafanikiwa kushinda
pambano lake dhidi ya bondia wa Australia, Jeff Horn.
Pambano
hilo ambalo litafanyika mjini hapa mnamo Jumapili Julai 2, mwaka huu,
linatarajiwa kuwa la aina yake kutokana na rekodi nzuri ya mpinzani huyo wa
Pacquiao ambaye hakuwahi kupoteza pambano lolote.
Ili kunogesha
pambano hilo zaidi, kambi ya Mfilipino huyo aliye chini ya kocha Freddie Roach,
tayari imeeleza kwamba imeshafanya mazungumzo na kambi ya Mayweather na ushindi
wa Pacquiao ambaye anatakiwa ashinde kwa KO, utaharakisha kukamilika kwa
marudiano ya mabondia hao.
“Tunafukuzia
pambano la marudiano na Mayweather na tunajua kuwa (Pacquiao) akishinda kwa KO,
itakuwa fursa nzuri ya kufanikisha pambano hilo la marudiano. Ushindi kwenye
pambano hili, itakuwa kitu kizuri zaidi,”
“Nafahamu
kwamba atashinda pambano hilo tena kwa KO, kitu ambacho nimekuwa nikikisubiri
kwa muda mrefu na natarajia kitatokea siku hiyo,” alisema kocha Roach.
Hata hivo,
pambano hilo linatarajiwa kuwa gumu zaidi kutokana na rekodi nzuri aliyonayo
Horn ambaye ana taaluma ya ualimu.
Courier
Mail
No comments