Header Ads

Matumizi ya nguvu kupita kiasi dhidi ya waandamanaji yamponza IGP wa Venezuela



Antonio Benavides anasema ni vigumu kutumia njia ya kawaida kuwakabili waandamanaji wasiochoka 
Antonio Benavides
CARACAS- OFISI ya Mwanasheria Mkuu wa Serikali nchini, imemtaka Mkuu wa zamani wa Jeshi la Polisi, Antonio Benavides kutoa maelezo juu ya matumizi ya nguvu zilizopitiliza dhidi ya waandamanaji wanaoipinga Serikali.

Ofisi hiyo, imesema kuwa kuna ushahidi wa kutosha juu ya matumizi ya nguvu zilizopitiliza kwa waandamanaji. Benavides anatarajiwa kuhojiwa siku ya Julai 6, mwaka huu.
Aliondolewa madarakani wiki iliyopita, baada ya polisi aliowapa maelekezo kuonekana wakiwafyatulia risasi waandamanaji. Zaidi ya watu 80 wameuawa, katika maandamano ya miezi mitatu ya kupinga utawala wa Rais Nicolas Maduro.


No comments

Powered by Blogger.