Mwanamke amuua mpenziwe kwa mzaha wa YouTube

MINESOTTA-
MWANAMKE mmoja mjini hapa, amekamatwa kwa kumpiga risasi na kumuua mpenzi wake
katika kile kinachosemekana ni mgogoro wa mtandaoni.
Monalisa
Perez mwenye umri wa miaka 19, amewekwa kizuizini baada ya kumpiga risasi Pedro
Ruiz alipokuwa akishikilia kitabu katika kifua chake akidhani kitazuia risasi
hiyo.
Wawili hao
wana mtoto wa miaka mitatu na takriban watu 30 walikuwa wakiangalia video hiyo
ya YouTube alipompiga risasi mpenziwe.
Shangazi yake
Ruiz anasema kuwa, walifanya kitendo hicho ili kuimarisha ufuasi wao katika
katika mitandao ya kijamii.
Claudia Ruiz
aliambia runinga ya WDAY-TV kwamba binamu yake alimwambia kwamba alitaka
kufanya kitendo hicho ‘kwa sababu walihitaji kupata wafuasi zaidi, na kuongeza
kuwa walidai ‘tunataka kuwa maarufu’.
“Aliniambia
kuhusu wazo hilo na nikamwambia, ‘Musafanye hivyo’. Kwa nini utumie bunduki?
Kwa nini?” Claudia Ruiz alikiambia chombo hicho cha habari.
“Walikuwa
wakipendana sana. Ulikuwa mzaha uliofanyika kimakosa” alisema Claudia Ruiz.
No comments