Header Ads

Makosa matano ambayo wanatuhumiwa Rais wa Simba na Makamu wake

Alhamisi ya June 29 2017 Rais wa club ya Simba Evans Aveva na makamu wake Geofrey Nyange Kaburu walifikishwa Mahakama ya hakimu mkazi Kisutu Dar es Salaam kusikiliza mashitaka yao.

Evans Aveva na Kaburu wameshtakiwa kwa makosa kwa matano ambayo kwa mujibu ya sheria yanawanyima dhamana hivyo wamelazimika kwenda lumande hadi July 13 ndio kesi yao itaendelea chini hakimu Victoria Nongwa.
Kutoka kulia ni Rais wa Simba Evans Aveva na wa pili kulia ni makamu wa Rais wa Simba, Geofrey Nyange 'Kaburu'
Makosa matano wanayotuhumiwa nayo viongozi wa Simba
1- March 5 2016 Evans Aveva anatuhumiwa kugushi nyaraka za kuidai Simba dola 300,000 za kimarekani ambazo ni zaidi ya Tsh milioni 600.
2-March 16 zilitumika nyaraka za uongo kujilipa deni kupitia bank ya CRDB Azikiwe.
3- Kula njama na kutakatisha fedha kinyume cha sheria kiasi cha dola 300,000 za kimarekani.
 

4- Kosa la nne Evans Aveva anatuhumiwa kutakatisha fedha ambazo alizipokea kupitia bank ya Barclays tawi la Mikocheni.
5- Kaburu anatuhumiwa pia kumsaidia Evans Aveva kutakatisha fedha dola za kimarekani 300000 kupitia Bank ya Barclays tawi la Mikocheni.
Makamu wa Rais wa Simba Kaburu mwenye shati jekundu akiongea na wakili
Kwa mujibu wa sheria makosa ya kutakatisha fedha hayana dhamana hivyo Rais wa Simba Evans Aveva na makamu wake Geofrey Nyange Kaburu watakuwa lumande hadi July 13.
Chanzo; Millard Ayo

 

No comments

Powered by Blogger.