Header Ads

Afungua kesi mahakamani kutaka Raila Odinga azuiliwe kugombea urais Kenya



Man wants Raila barred from August polls terming his degree questionable
NAIROBI- MTU mmoja jijini hapa, amefungua shauri mahakamani ambalo linataka mgombea urais kupitia Muungano wa Vyama vya Upinzani Kenya (NASA), Raila Odinga kuzuiwa kuwania nafasi hiyo Agosti 8 mwaka huu.

Shauri hilo liliwasilishwa mahakamani na Charles Ndungu Mwangi, ambaye ameitaka mahakama kumtaka Waziri wa Elimu nchini, Dk Fred Matiang’i kuwasilisha mahakamani hapo vyeti vya elimu vya shule ya msingi, sekondari na kile cha shahada ya uhandisi cha kiongozi huyo.
“Kiongozi wa upinzani hayuko juu ya Katiba na sheria ya Kenya na anapaswa kuiheshimu, kuitunza na kuilinda na kushindwa kufanya hivyo kutasababisha yeye ajaribu kutengeneza Serikali isiyo halali,” alidai mlalamikaji.
Katika shauri hilo, mlalamikaji amewajumuisha pia Mwenyekiti wa Tume Huru ya Uchaguzi nchini (IEBC), Wafula Chebukati; Mwenyekiti wa EACC, Eliud Wabukala; Mkuu wa Jeshi la Polisi, Joseph Boinett; Mwanasheria Mkuu wa Serikali na Waziri wa Elimu.
Mlalamikaji huyo alidai kuwa Waziri wa Elimu ameshindwa kutoa kwa umma taarifa kamili za elimu ya Raila.


No comments

Powered by Blogger.