Header Ads

Kiongozi wa upinzani Urusi atupwa jela



Alexei Navalny (right) speaks after a hearing in a court in Moscow. Photo: 12 June 2017
MOSCOW- KIONGOZI wa upinzani nchini, Alexei Navalny amehukumiwa kifungo cha siku 30 jela kwa kukiuka sheria baada ya kuandaa maandamano.

Navalny (pichani) alikamatwa nyumbani kwake mjini hapa jana, kabla ya kufanyika kwa maandamano ya kupinga ufisadi nchini. Mamia ya watu walikamatwa wakati wa maandamano hayo yaliyofanyika kote nchini.
Polisi wa kupambana na maandamano, walikuwa wakiwakamata waandamanaji kutoka kwa umati, kwa mujibu wa mwandjshi wa BBC aliyekuweko.
Mahakama ilitangaza umuzi wake jana, na kukataa wito wa mawakili wa Navalny kufuta kesi hiyo. Kiongozi huyo wa upinzani mwenye umri wa miaka 42, baadaye alithibitisha hukumu yake katika mtandao wa Twitter.
Polisi mjini hapa wanasema kuwa takriban watu 5000 walishiriki maandamano hayo.

No comments

Powered by Blogger.