Header Ads

Jengo la ghorofa 7 laporomoka Nairobi



Collapsed building in Nairobi
NAIROBI- WATU zaidi ya 15 hawajulikani walipo, baada ya jengo la ghorofa 7 kuporomoka ghafla usiku wa kuamkia leo katika mtaa wa Kware Pipeline Embakasi, jijini hapa.

Kwa mujibu wa taarifa iliyotolewa na Shirika la Msalaba Mwekundu nchini, kupitia akaunti yao ya Twitter, kikosi kazi cha uokozi cha shirika hilo tayari kipo eneo la tukio kwa ajili ya shughuli za uokozi.
Taarifa nyingine ya gazeti la Star, ilieleza kwamba watu wengi wameokolewa kutoka kwenye jengo hilo.
BBC

No comments

Powered by Blogger.