Header Ads

Amri ya Trump yagonga mwamba tena



Trump
WASHINGTON DC - MAHAKAMA ya Rufaa nchini, imemua kuwa uamuzi wa kuzuia mpango uliofanyiwa marekebisho wa marufuku ya Rais Donald Trump, kuzuia watu kutoka nchi sita za Kiislamu haistahili kuwepo.

Wakitoa hukumu kufuatia kesi iliyowasilishwa na jimbo la Hawaii, majaji walieleza kuwa amri hiyo kuu inakiuka sheria zilizopo za uhamiaji.
Rufaa hiyo iliyowasilishwa katika Mahakama ya Rufaa ya San Fransisco, ni kufuatia umamuzi uliotolewa kupinga raia ambao wengi wao wakiwa wa nchi za Kiislam kuingia Marekani.
Hata hivyo, mahakama haikusema kuwa Serikali inatakiwa kuzipitia upya taratibu za ukaguzi kwa watu wanaoingia nchini.
Msemaji wa Ikulu, Sean Spicer ameutetea msimamo huo wa Rais Trump, akisistiza kuwa kila lilalowezekana linatakiwa kufanywa kwa ajili ya ulinzi wa Marekani
“Nadhan wote tunafahamu kuwa hizi ni nyakati za hatari dhidi ya tishio la ugaidi, tunapaswa kulinda kuingia kwa watu wanaoweza kufanya vitendo vya ugaidi na umwagaji damu. Tunaendelea kuwa na imani kwamba, amri za rais wetu ni kwa mujibu sheria na kwamba tunaamini mahakama ya juu itazipitisha,” alisema Spicer.
Hata hivyo, Mwanasheria Mkuu wa jimbo la Maryland na Columbia, Brian Frosh amefungua mashitaka dhidi ya Rais Trump kwa madai ya kupokea malipo ya nje kupitia makampuni yake.
Akizungumza na waandishi wa habari mjini hapa, Frosh ambaye anatokea kampuni ya Maryland's Attorney Generel, aliseama Trump kujihusisha biashara akiwa madarakani ni kuvunja katiba
“Aliiteuwa hoteli yake ya kimataifa ya Trump kwaajili ya wanadiplomasia na maofisa wa Serikali. Amekuwa akionekana kwenye sehemu nyingi za biashara zake na imekuwa kama sehemu ya kutangaza biashara hizo.
Analipwa na makampuni yanayo milikiwa na nchi za nje kama vile China, ambao pia ni wapangaji katika majengo yake. Na amekuwa akiendelea kuchukua malipo kutoka nchi za Saudi Arabia, India, Afghanistan na Qatar nchi ambazo zina hisa majengo yake ya kibiashara yajulikanayo kama Trump World Tower,” alisema Frosh.
Rais Trump amekuwa akikabiliwa na upinzani mkali, kufuatia baadhi ya maamuzi ambayo amekuwa akiyafanya tangu kuingia madarakani, ikiwemo hatua hii aliyoichukua kupiga marufuku raia kutoka baadhi ya nchi za Kiislam kuingia Marekani.


No comments

Powered by Blogger.