Header Ads

Daktari atuhumiwa kupandikiza mbegu zake kwa wanawake Uholanzi



Mmoja wa watu wanaodhania walizaliwa kwa mbegu ya daktari Jan Karbaat
Walalamikaji na baadhi ya watoto waliozaliwa kwa njia ya upandikizaji
AMSTERDAM, Uholanzi
MAHAKAMA nchini, imeidhinisha ombi la familia zinazotaka vipimo vya vinasaba (DNA) vichukuliwe juu ya mmiliki wa kliniki ya uzazi ya daktari anayeshutumiwa kutumia mbegu zake za kiume katika makumi kupandikiza wanawake wanaotafuta mbegu za kiume.

Daktari huyo, Jan Karbaat anashukiwa kuwa baba wa watoto wapatao 60, katika kituo cha afya alichomiliki katika eneo la Bijdorp, karibu na Rotterdam.
Vipimo sasa vitafanyika juu ya vifaa vilivyochukuliwa kutoka kwenye nyumba yake baada ya kifo chake Aprili mwaka huu, akiwa na umri wa miaka 89.
Wakili wa familia yake anasema hakuna ushahidi wa kuthibitisha madai hayo. Jan Karbaat alijiita ‘muasisi wa fani ya uzazi wa kusaidiwa’.
Kliniki yake ilifungwa mwaka 2009, wakati kulipokuwa na taarifa kwamba alidaiwa kugushi data, uchunguzi na maelezo ya watoaji wa mbegu za kiume na kuzidisha idadi inayoruhusiwa ya idadi ya watoto sita kwa kila anayejitolea kutoa mbegu za uzazi.
Katika kesi mahakamani mwezi uliopita, wakili wa wazazi 22 na watoto walisema kwamba visa vinavyoshukiwa vinajumuisha mtoto wa mteja wao mwenye macho ya hudhurungi wakati alikuwa na macho ya blu na mvulana wa mteja wakebambaye anasura inayofanana na daktari.
Taarifa za DNA zitasalia kuwa siri hadi pale watoto watakapoonesha kuwa kuna sababu za kuamini daktari alikuwa baba yao, kulingana na mwandishi wa BBC Anna Holligan, ambaye alikuwa katika mahakama ya wilaya ya Rotterdam.
Hatimaye, kama taarifa za DNA zitawiana na watoto hao ambao wengi wao walizaliwa miaka ya 1980, kutakuwa na tumaini la kumshitaki daktari, labda kwa misingi ya kwamba hawangepaswa kuwepo.
Joey, ambaye anaamini Jan Karbaat huenda ni baba yake aliiambia BBC: “Ina maana kubwa kwangu ... Tunatumai kupata majibu.”
Wakili wa familia ya Karbaat anapinga kufanyika kwa vipimo vyovyote vya vinasaba DNA. Wakati wa uhai wake, daktari mwenyewe alikataa kufanya vipimo hivyo.
Hata hivyo, mwezi uliopita, mtoto wa Karbaat alitoa vinasaba vyake ili vipimwe ambavyo vilionesha kuwa baba yake anaweza kuwa baba wa watoto 19, waliozaliwa kwa njia ya uzazi wa kutungishwa mbegu kwa lugha ya kitaaamu IVF, kulingana na ripoti ya shirika la habari la AFP.

No comments

Powered by Blogger.