Trump alaumiwa kwa uamuzi wake
Mahama (pichani)
alituma ujumbe wake kwa njia ya Twitter, akiutaja uamuzi wa Trump wa kujiondoa
kwenye makataba huo wa mazingira kama “Jambo ambalo ni vigumu kuliamini. Ni
siku ya huzuni sana katika ushirikiano wa kimataifa.”
Rais
huyo wa zamani alikuwa ni miongoni mwa viongozi wa dunia waliounga mkono
makubaliano hayo ya kihistoria juu ya mazingira mjini Paris, akiahidi
kutekeleza hatua za kupunguza hewa ya makaa duniani.
Alitwitt
kwamba Marekani imejiondoa katika uongozi wake wa dunia. Trump alisema kuwa
mkataba huo ‘uliiadhibu’ Marekani na utasababisha kupotea kwa mamilioni ya
ajira nchini humo.
Wakati
huo huo, aliyekuwa Katibu Mkuu wa Umoja wa Mataifa Koffi Annan ambaye ni Mwenyekiti
wa Baraza la Wazee wa Afrika alisema: “Mabadiliko ya hali ya hewa ni tisho
kubwa la enzi yetu, Makubaliano ya Paris ni matokeo ya makubaliano mengi ya
ushirikiano na utashi wa kutafuta suluhu ya pamoja ya tatizo la dunia.
Hakuna
nchi moja inayoweza kuvuruga makubaliano. Wakati Marekani inajiondoa
inadhoofisha mkataba huo wa kimataifa, haitauvunja,” alisema Annan.
“Kilichosalia
kwa mkataba wa Paris ni kwa pande zilizosalia kuendelea kujitolea kuongeza
juhudi za kutatua matatizo ya mabadiliko ya tabia nchi,” Annan aliandika kwa
niaba ya wajumbe wa Baraza la Wazee wa Afrika.
Ndani
ya Marekani kwenyewe, biashara na mamlaka za majimbo zinaweza na lazima
zikchukue hatua pale serikali ya shirikisho itakaojiondoa, waliongeza.
No comments