Header Ads

Mwanafunzi Mwingereza asimulia maisha yalivyo Korea Kaskazini

Chai
Benjamin Griffin akijumuika na wenzake kupata ‘kikombe cha chai’ katika jumba la urafiki wa kimataifa nchini Korea Kaskazini.
LONDON, Uingereza
KOREA Kaskazini inapotajwa, linalotokea akilini mwa watu wengi huwa ni ubabe wa taifa hilo na majaribio ya makombora na silaha za nyuklia, pamoja na kiongozi wake, Kim Jong-un.

Aidha, mara kwa mara taarifa za raia wa nchi za Magharibi kukamatwa na kufungwa jela huripotiwa. Lakini sasa kuna mwanafunzi Mwingereza, ambaye anaamini wengi hawajalifahamu vema taifa hilo.
Badala ya kuitenga Korea Kaskazini, anaamini wakati umefika kwa watu kufanya urafiki na taifa hilo.
“Tumekuwa wepesi wa kuibandika Korea Kaskazini maneno kama vile ‘marufuku’, ‘taifa lenye usiri mkubwa’, ‘dhiki’, 'ukatili’ na kadhalika, lakini nataka kuondoa dhana hiyo, angalau kwa dakika moja, tuitazame Korea Kaskazini katika ngazi ya utu,” anasema Benjamin Griffin, mwenye umri wa miaka 24.
Kabla yake kufanya ziara yake ya kwanza nchini humo miaka minne iliyopita, ufahamu wake kuhusu nchi hiyo anasema ulitokana na ‘makala moja pekee aliyokuwa ameitazama na video fupi za YouTube.’
Lakini alipata nafasi ya kusafiri taifa hilo kwa kutumia shirika lakitalii la Juche Travel Services (JTS), safari iliyomfumbua macho.
Students at the tourism college
Benjamin (mwenye tai ya bluu) akiwa na wanafunzi wa utalii ambao anawafundisha nchini Korea Kaskazini.
“Nilipoiona Pyongyang kwa mara ya kwanza mwaka 2013, nilitarajia kuwaona wanajeshi kila nilikoenda. Ni kana kwamba sikuwa nawatazama kama watu halisi,”
“Lakini ukweli ni kwamba tuliwaona watu wakitembea kwenda kazini, kwenda madukani na kucheza ngoma katika bustani. Kwa kiasi fulani, nilishangazwa na maisha hayo ya kawaida.
“Ukweli ni kwamba, katika maisha ya kila siku ya raia wa Pyongyang, huwa hawana wasiwasi kuhusu njia gani bora ya kukabiliana na ubabe wa Marekani au maovu ya mfumo wa ubepari. Wanachokijali zaidi ni, 'Nitaenda wapi dukani kununua bidhaa? Nimefikia wapi katika kazi yangu? Binti yangu ataolewa?” anasema Benjamin.
Mwaka uliofuata, akiwa na miaka 21, alirejea huko kama mwalimu wa kujitolea wa somo la Kiingereza katika chuo cha utalii cha Pyongyang.
Baadaye, alihitimu na kuwa mwelekezi wa watalii wa TJS na sasa ameanzisha mpango wa kuwasaidia watu wa kila tabaka au asili wanaotaka kwenda kukaa chuo kikuu cha Kim Il-sung, Julai mwaka huu.
Washiriki watalala katika mabweni ya chuo na kujifunza Kikorea kwa masaa manne kila siku.
Muda huo mwingine watautumia kwa kutembea, kujionea mji na vivutio mbalimbali, na kisha kushiriki katika shughuli mbalimbali kama vile kuogelea, kucheza ngoma asili na kucheza mchezo wa kandadna wa wachezaji watano kila upande.
Aidha, kutakua pia na fursa ya kukutana na baadhi ya raia wa Korea Kaskazini, ingawa raia hao watakua wamechunguzwa kikamilifu.
“Hatuwezi kamwe kusahau matatizo yaliyopo Korea Kaskazini, lakini tunafaa kua na uelewa fulani. Utalii wa elimu unasaidia hilo. Sitaki kuacha kuuliza maswali, lakini ni muhimu pia kuifahamu nchi hiyo kikamilifu, watu wake na thamani na maadili yao.
“Ni kweli kuna siasa - wana majaribio yao ya silaha za nyuklia, na ukiukwaji wa haki za kibinadamu - lakini ni muhimu kuangazia uhusiano wa binadamu mmoja na mwingine.” Anasema Benjamin.
Ben
Benjamin akifundisha wanafunzi somo la Kingereza katika Chuo Kikuu cha Utalii nchini Korea Kaskazini.
Benjamin Griffin outside the Palace of the Sun, the mausoleum of Kim Il-sung

Benjamin Griffin akiwa mbele ya kaburi la Kim II-sung nchini Korea Kaskazini.





No comments

Powered by Blogger.