Header Ads

Jinping awasili Hong Kong kuadhimisha miaka 20 ya utawala wa China



President Xi Jinping arrives in Hong Kong with his wife
HONG KONG- LICHA ya harakati mbalimbali za kudai uhuru kamili wa Hong Kong kutoka China, Rais Xi Jinping amewasili mjini hapa ili kuadhimisha miaka 20 tangu China ilipokabidhiwa utawala kamili juu ya Hong Kong.

Akizungumza mbele ya halaiki iliyojitokeza uwanja wa ndege kumlaki, Rais Jinping alisema kwamba; “Baada ya miaka 9, hatimaye tena naikanyaga ardhi ya Hong Kong. Ninajisikia furaha isiyo na kifani, kwani Hong Kong imekuwa na sehemu kwenye moyo wangu muda wote.”
Hata hivyo, ujio wa Rais Jinping mjini hapa haukufurahiwa na watu wote kwani kabla ya ujio huo mamia ya wanaharakati na waandamanaji ambao wamekuwa wakidai uhuru kamili wa Hong Kong wamekamatwa na kuwekwa ndani ili wasivuruge sherehe hizo zinazotarajiwa kufanyika Jumamosi.
Miaka 20 iliyopita, utawala wa Uingereza uliirudisha Hong Kong katika mikono ya China chini ya mfumo ujulikanao kama ‘Taifa moja, Mifumo miwili’ ambao unaipa mamlaka China ya kuitawala Hong Kong kiuchumi na kiutawala.
SkyNews

No comments

Powered by Blogger.