WHO kukabiliana na mlipuko wa Ebola DRC

Wataalam wa Shirika la Afya Duniani (WHO) wa kupambana na Ebola, wakiwa kazini.
GENEVA,
Uswisi
SHIRIKA la
Afya Duniani, WHO limeahidi kuchukua hatua za tahadhari za haraka zaidi, ili
kuzima mlipuko wa ugonjwa hatari wa Ebola ambao umetokea katika maeneo ya Kaskazini
mwa Jamuhuri ya Kidemokrasi ya Congo (DRC).
Kwa mujibu
wa taarifa kutoka WHO, wataalamu wa kiufundi wa shirika hilo wametumwa hadi
maeneo ya vijijini, kunakoaminika kutokea visa 11 vya ugonjwa wa Ebola zikiwemo
ripoti ya vifo vya watu watatu.
Taarifa hiyo
imeeleza kuwa wataalam hao wanafanya kila mbinu kubaini upana wa mlipuko wa
ugonjwa huo, kuwapa tiba walioambukizwa virusi vya ugonjwa huo, na kuwatambua
walioambukizwa au watu waliokaribiana na walioambukizwa virusi hivyo.
Huu ni
mlipuko wa 8 uliotambuliwa wa Ebola nchini DRC, tangu kisa cha kwanza cha Ebola
kutambuliwa nchini humo mnamo mwaka wa 1976.
No comments