Header Ads

Korea Kaskazini yafanya majaribio ya makombora masafa marefu



https://ichef-1.bbci.co.uk/news/660/cpsprodpb/16E9E/production/_96045839_571c99dd-2bd3-4627-9337-ae8fd882bf10.jpg
Magari ya kivita yakiwa na makombora ya masafa marefu yalipokuwa yakioneshwa siku ya maonesho ya kijeshi hivi karibuni nchini Korea Kaskazini. Makombora hayo yamefanyiwa majaribio na kuibua shutuma kote duniani.
SEOUL, Korea Kusini
WAKATI Mjumbe Maalum wa Wizara ya Mambo ya Nje wa Korea Kaskazini, Choe Son Hui akisema kuwa endapo mazingira yakiruhusu watazungumza na Marekani, taifa hilo limefanyia majaribio makombora ya masafa marefu.

Hatua hiyo ya kufanya majaribio ya makombora hayo na zana za nyuklia, imeibua shutuma nyingi kote duniani kulaani majaribio hayo yenye lengo la kuendelea kuleta hali ya wasiwasi.
Marekani imetaka vikwazo zaidi viongezewe kwa taifa hilo, huku Ikulu ya White House ikisema kuwa, Korea Kaskazini imeachwa kutekeleza upumbavu kwa muda mrefu.
Rais mpya wa Korea Kusini, Moon Jae-in, amelaani kitendo hicho cha Korea Kaskazini cha kufanya majaribio zaidi zana zake za mafasa marefu, akilitaja kama kitendo cha uchochezi.
Jeshi la Marekani limetihibtisha kuwa kombora hilo la masafa marefu, lilirushwa karibu na mji wa Kaskazini Magharibi wa Kusong na kuanguka katika bahari ya Japan.
Moon ambaye alisema anataka ushirikiano zaidi na utawala wa Korea Kaskazini, wakati wa kampeni zake, amejibu hatua hiyo kwa kuitisha mkutano wa dharura na washauri wake wa kiusalama.
Jaribio lingine la Korea Kaskazini la kuifanyia majaribio zana hizo, liligonga mwamba wiki mbili zilizopita. Korea Kaskazini imekiuka maazimio ya Umoja wa Mataifa pamoja na vikwazo na kufanya majaribio matano ya zana zake za masafa marefu za nuklia.

No comments

Powered by Blogger.