Aamua kujioa kutimiza ndoto zake

TAIPEI, Taiwan
MWANAMKE mmoja
ambaye anaugua saratani ya matiti, amefikia uamuzi wa kujioa mwenyewe baada ya
kusubiri kupata mchumba kwa muda mrefu.
May Chen
mwenye umri wa miaka 28 kutoka Taiwan, aliiambia BBC kwamba anaugua ugonjwa huo
lakini hajakubali sababu hiyo kuhujumu ndoto yake ya kuolewa.

“Nimekuwa
nikisubiri mtu (mwanaume) ajitokeze na kusema kwamba angependa kufunga ndoa nami,
mbali na kupiga picha za harusi nami,” Chen aliiambia BBC.
Alisema
kwamba, wakati unapohisi kwamba huna miaka mingi ya kuishi huna budi kujifanyia
masuala muhimu ili kutimiza ndoto zako. Anasema kwamba aliamua kuafikia ndoto
yake kupitia kupiga picha za harusi. Alijichagulia marinda yote manne na vito
alivyovaa.
Chen anadai
kuwa wapiga picha walimshauri kupiga picha katika studio, lakini yeye
akawaambia kwamba anataka picha zilizo sawa na zile za harusi. Alisema aliamua
kukodisha gari na kwenda kupiga picha hizo katika maandhari ya harusi.
“Nilipovalia
rinda la harusi nilijawa na hisia mpaka nikahisi kulia. Nilihisi kana kwamba nimeafikia
ndoto yake ya miaka mingi,” alisema Chen.
Kutokana na
kuugua saratani ya matiti, Chen hulazimika kwenda hospitali mara tatu kwa wiki
ili kudungwa sindano mbali na kutibiwa kwa kutumia kemikali.
Chen
anabainisha kwamba, kwa muda mrefu hakuweza kusimama kwa miguu miwili na kuvaa
suruali ndefu, kutokana na kulazimika kutembea kwa kutumia kiti cha magurudumu.
Anasema
kwamba hakuweza kutembea na kwamba nywele alizo nazo sio nywele zake asilia. Habari
ya mwanamke huo imewagusa watu wengi ulimwenguni.

No comments