Header Ads

Wafungwa 17 wauawa kwa risasi Papua New Guinea



Mwaka 2016 inadaiwa kuwa wafungwa walivamia lango kuu la gereza hilo
Gereaza la Buimo mjini Lae, ambalo wafungwa wake zaidi ya 70 walitoroka mwishoni mwa wiki.
LAE, Papua New Guinea
MAOFISA wa magereza nchini, wamewapiga risasi na kuwauwa wafungwa 17, ambao walivunja gereza na kutoroka mwishoni mwa wiki.

Aidha, taarifa zaidi zinaeleza kuwa Polisi wamewatia mbaroni wafungwa watatu, huku wakiendelea kuwasaka wengine 50 ambao bado hawajulikani waliko tangu kutokea kwa kisa hicho katika gereza la Buimo katika mjini hapa.  
Polisi walisema kuwa, wengi wa wafungwa waliotoroka walikuwa wahalifu sugu. Idara ya usalama nchini imewatahadharisha raia kuwa macho na watoe taarifa kwa vyombo vya usalama pindi wakiwaona wafungwa hao.
Gereza hilo la Buimo huwa na msongamano mkubwa wa wafungwa na uchafu, na mwaka jana wafungwa 12 waliuawa baada ya kujaribu kutoroka.

No comments

Powered by Blogger.