Header Ads

Trump atakiwa kusalimisha kanda za mazungumzo yake na Comey



Donald Trump ametakiwa kusalimisha kanda za mazungumzo yaliorekodiwa kati yake na aliyekuwa mkuu wa FBI James Comey
Rais wa Marekani, Donald Trump
WASHINGTON DC, Marekani
WABUNGE wandamizi nchini, wamemtaka Rais Donald Trump kusalimisha mazungumzo yoyote yaliyorekodiwa kati yake na aliyekuwa mkurugenzi wa shirika la FBI, James Comey aliyemfuta kazi.

Kiongozi wa Democrats katika bunge la seneti, Charles Schumer alionya kuwa uharibifu wa kanda hizo utakuwa uvunjaji wa sheria.
Naye Seneta wa Republican Lindset Graham alisema kuwa Ikulu ya Whitehouse inahitaji kuwa wazi kuhusu iwapo kulikuwa na kanda zozote za rekodi za mazungumzo hayo au la.
Mwito huo unajiri baada ya Rais Trump kuandika maneno katika mtandao wake wa Twitter, yanayoonekana kuwa vitisho kwa mkuu huyo wa zamani wa FBI.
Alimuonya Comey wiki iliopita dhidi ya kuzungumza na vyombo vya habari, akisema anatumai hakuna rekodi za mazungumzo yao. Ikulu ya Whitehouse haijathibitisha wala kukana kuwepo kwa kanda hizo.
Schumer pia alionya kwamba masenata wa chama cha Democrats, watakataa kumuunga mkurugenzi mpya wa FBI hadi pale mtaalam atakapochaguliwa kuchunguza hatua ya Urusi kuingilia masuala ya Marekani katika uchaguzi uliopita.
FBI inachunguza madai hayo pamoja na ushirikiano wa Urusi na kampeni ya Rais Trump, licha ya kiongozi huyo kukanusha mara kwa mara kuhusu uhusiano wowote na aliongeza kuwa hakuna uhusiano wowote baina ya Comey kufutwa kazi na uchunguzi huo.
Anasema kuwa alimpiga kalamu Comey kwa sababu alikuwa ameshindwa kufanya kazi vizuri.  Wanachama wa Democrats wamemshutumu Trump kwa kumfuta kazi Comey ili kujaribu kusitisha uchunguzi wa FBI.
BBC

No comments

Powered by Blogger.