Header Ads

Korea Kaskazini yadai Hwasong 2 linabeba kichwa cha nyuklia



Image result for Hwasong 2 testing yesterday
PYONGYANG, Korea Kaskazini
SERIKALI imedai kwamba kombora la masafa marefu la Hwasong 2, ambalo limefanyiwa majaribio jana, ni jipya na lina uwezo wa kubeba kichwa cha nyuklia.

Kombora hilo lililorushwa katika mji wa Kusong, lilienda angani urefu wa kilomita 2,000 na kusafiri kilomita 700 kabla ya kuangukia baharini Magharibi mwa Japan.
Jeshi la Korea Kusini limesema kuwa haliwezi kuthibitisha madai hayo ya Korea Kaskazini. Lakini limesema kuwa kombora hilo lilionekana kuweza kuruka angani, hatua ambayo ni muhimu katika utengenezaji wa makombora ya masafa marefu kulingana na kituo cha habari cha Yonhap.
Majaribio ya mara kwa mara ya makombora ya masafa marefu yanayofanywa na taifa hilo, yanakiuka vikwazo vya Umoja wa Mataifa (UN) na yamesababisha wasiwasi miongoni mwa jamii ya kimataifa pamoja na Marekani.
Marekani na Japan zimetaka kufanyika kwa mkutano wa dharura katika Baraza la Usalama la Umoja wa Mataifa mapema kesho.
Shirika la habari nchini (KCNA), limesema kwamba jaribio la kombora jipya la masafa marefu la Hwasong 12 lilifanyika kama ilivyopangwa. KCNA ilieleza kuwa jaribio hilo lililenga kuonesha kwamba kombora hilo jipya lina uwezo wa kubeba kichwa cha nyuklia.
BBC

No comments

Powered by Blogger.