Ufanisi wa vifaa vya kupima ubora wa afya watiliwa shaka

Hayo
ni kulingana na uchunguzi wa vifaa hivyo katika Chuo Kikuu cha Stanford cha Marekani.
Hata hivyo, imebainika kwamba vifaa hivyo vina uwezo wa kupima mapigo ya moyo
kwa ufasaha.
Watafiti
hao wamependekeza kwamba wanaoutumia vifaa hivyo wawe waangalifu hususan
wanapotumia vifaa hivyo kuchagua wanachokula.
Utafiti
huo umependekeza wanaotengeneza vifaa hivyo, kutoa maelezo kamili ya jinsi
wanavyotoa vipimo hivyo. Vifaa vilivyofanyiwa utafiti ni Apple Watch, Fitbit
Surge, Basis Peak, Microsoft Band, PulseOn na MIP Alpha 2.
Vifaa
hivyo vilipatikana kuwa na makosa ya zaidi ya 20% katika kupima viwango vya
nguvu ya mwili inayotumika katika mazoezi.
Daktari
Euan Ashley wa chuo hicho amesema watumiaji wa vifaa hivyo wanafaa kujuzwa
manufaa na upungufu wa vifaa hivyo vinavyovaliwa mikononi.
No comments