Header Ads

Ndege za Pakistan zatumiwa kusafirisha heroin hadi Uingereza

Heroin ilipatikana ndani ya dege ya Pakistan ambaye ingesafiri kuenda London

Ndege ya Shirika la Ndege la Pakistan (PIA)

KARACHI, Pakistan
SHIRIKA la ndege la Serikali nchini, limesema kuwa linachukua hatua kuhakikisha kuwa ndege zake hazitumiwi kubeba madawa ya kelevya baada ya dawa ya heroin, kupatikana kwenye ndege zake mbili zinazofanya safari kuenda mjini London.

Tarehe 15 mwezi huu, maofisa wa mipaka wa Uingereza walikamata ndege iliyokuwa ikitokea mjini Islamabad ilipowasili uwanja wa Heathrow mjini London na kuikagua kwa saa kadhaa.
Shirika la kukabiliana na uhalifu nchini Uingereza baadaye lilisema kuwa, kiwango fulani cha heroin kilipatikana kikiwa kimefichwa katika sehemu tofauti za ndege hiyo. Kuna madai kuwa utawala wa Uingereza ulichukua hatua hiyo kutokana na taarifa ilizopokea kutoka Pakistan.
Hakuna mtu aliyekamatwa lakini rubani wa ndege hiyo hakuruhusiwa kurudi Pakistan siku iliyofuata. Kisa hicho kilisabisha aibu kwa shirika la ndege la Pakistan, ambalo linapata nafuu baada ya ajali mbaya iliyowaua watu wengi Desemba, mwaka jana.
Mei 22 mwaka huu, maofisa wa Pakistan katika uwanja wa ndege wa Islamabad, walikamata zaidi ya kilo 20 za dawa ya heroin ndani ya ndege nyingine iliyokuwa isafiri kuenda Heathrow.
Kwa sasa uchunguzi unafanyika kubaini ikiwa kuna ushirikiano wa kutumiwa ndege za shirika la ndege la Pakistan, kusafirisha madawa ya kulevya kuenda nchi za ng'ambo.
BBC

No comments

Powered by Blogger.