Header Ads

Manowari ya Marekani yapita karibu na visiwa vya China




Uchina imetengeneza vituo vya oparesheni za kijeshi katika mwamba wa Mischief, katika bahari ya kusini mwa China
JAKARTA, Indonesia
MAOFISA wa Marekani wamesema kuwa, manowari ya wanamaji wa Jeshi la Marekani imetekeleza oparesheni maalum ya ‘uhuru wa ubaharia’ karibu na visiwa vinavyozozaniwa vya bahari ya Kusini mwa China.

Oparesheni hiyo karibu na kisiwa kimoja bandia kilichojengwa na China, inalenga kupinga madai ya taifa hilo la Asia kumiliki eneo hilo. China inadai umiliki wa visiwa na miamba ya baahari ya Kusini mwa nchi hiyo.
Mataifa mengine pia yanadai umiliki wa visiwa hivyo pamoja na miamba. Marekani imekuwa ikisisitiza kwamba ina uhuru wa kutekeleza oparesheni zake katika maeneo yoyote kwenye maji ya kimataifa.
Oparesheni hiyo imefanyika karibu na visiwa cha Spratley, ambayo China imejenga kambi ya kijeshi, jambo ambalo limezua ghadhabu miongoni mwa mataifa jirani.
Oparesheni hiyo ni ya kwanza tangu kuanza utawala wa Rais Donald Trump, na inalenga kukabiliana na majaribio ya China ya kudhibiti eneo, ambalo huwa linashuhudia shughuli nyingi za ubaharia.
Kumekuwa na vita baridi kati ya China na Marekani, ambapo kumekuwa na lawama kuwa eneo hilo linageuzwa kuwa la kijeshi.
Hatua hiyo ya Marekani itaathiri pakubwa uhusiano wake na China, hususan wakati ambapo utawala wa Trump unataka ushirikiano wa China katika kukabiliana na vitisho vya mashambulizi ya kinyuklia ya Korea Kaskazini

No comments

Powered by Blogger.